Katika sehemu hii tutazungumzia; kazi katika kuandaa shamba, matumizi ya moto, njia za kulima na zana za kulimia, mahitaji ya mahindi (udongo unaofaa na hali ya hewa inayofaa) na vitu vinavyosababisha rutuba kupotea kutoka kwenye shamba.
Tunasema shamba halina rutuba kwa kilimo cha zao fulani kama udongo wa hilo shamba hauna sifa za kuuwezesha mmea kupata virutubisho vinavyotakiwa kwa kiwango sahihi kuuwezesha kuota na kustawi. Rutuba (virutubisho) katika udongo huongezeka tunapoweka mbolea za asili au za viwandani. Virutubisho hivyo hupotea au hupungua kupitia njia zifuatazo;
![]() |
![]() |
Mmomonyoko wa udongo | Mafuriko huweza kuondoa rutuba kutoka sehemu moja kwenda ingine |
![]() |
![]() |
Kuvuna na pia kuvuna na kuondoa mabaki ya mavuno shambani | Kuchoma mabaki ya mavuno |