Mwanzo Kuandaa Shamba Mbegu & Kupanda Kutunza Shamba Kuvuna & Kuhifadhi Maswali | Majadiliano Mawasiliano & Ushauri Uza na Kununua

Kutunza Shamba

Sehemu hii tutazungumzia jinsi ya kutunza shamba la mahindi ambapo tutagusia mambo makuu manne (4) ambayo ni; nyasi na magugu shambani, mbolea, wadudu shambani, pamoja na matumizi ya kemikali shambani. Mambo haya manne yamefafanuliwa zaidi hapa chini.

Mambo ya kuzingatia kuhusu mbolea

Zingatia yafuatayo kuhusu mbolea;
  • Matumizi sahihi ya mbolea shambani huongeza rutuba kwenye shamba
  • Shamba lenye rutuba inayofaa kwa kilimo cha zao fulani hutoa mazao mengi na bora
  • Mmea wa mahindi hupitia hatua mablimbali za ukuaji mpaka kuvunwa na katika kila hatua huhitaji kiasi/ kiwango tofauti cha virutubisho hivyo inatakiwa mbolea kuwekwa kiwango/ kiasi sahihi katika wakati sahihi wa ukuaji wake
  • Mbolea tofauti zana viwango tofauti vya virutubisho. Baadhi ya virutibisho vya mahindi vilivyo kwenye mbole ni kama; Nitrogen, Phosphorus, Potassium, Magnesium, Calcium, Sulfur, Boron, Copper, Iron, Manganese na Zinc
  • Zao la mahindi huhitaji kiwango kikubwa zaidi cha Nitrogen, Phosphorus, na Potassium
  • Kukosekana kwa moja ya virutubisho hivyo tajwa husababisha mmea wa mahindi kuonyesha dalili fulani na kama virutubisho havitaongezwa mkulima hatopata mazao mengi na bora
  • Virutubisho vya mmea wa mahindi huweza kupatikana kwenye udongo wa shamba lenyewe, mbolea za asili au mbolea za viwandani

Juu ya Mbolea (virutubisho) shambani pia soma; Mambo muhimu kuhusu mbolea, Kujua uhitaji wa mbolea, Virutubisho vikuu na virutubisho vidogovidogo, Mambo ya kuzingatia kuhusu mbolea, Matumizi ya mbolea za asili, na Kilimo mzunguko.